Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA) imewataka wasanii kushirikiana nao katika operesheni waliyoanzisha kuhakikisha wanadhibiti watu wanaodurufu kazi zao ili ziweze kurudi kwenye mstari na kupata mapato.
Aidha, imesema TRA inataka kuboresha mfumo wa utoaji stampu ziwe za kielektroniki na kuachana na za karatasi ili ziwe bora zaidi katika bidhaa zote.
Hayo yalibainishwa Dar es Salaam jana na Mkurugenzi wa tafiti na sera wa (TRA), Tonedeus Muganyizi katika Maonesho ya 38 ya Biashara Kimataifa yanayofanyika katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere katika barabara ya Kilwa maarufu kama Sabasaba.
Alisema mwitikio wa wasanii bado uko chini hasa wasanii wa muziki katika kupambana na watu hao kwani hawajawa na mwamko wa kuweka kazi zao stampu lakini wasanii wakubwa wa filamu wamekuwa na mwamko na uelewa juu ya suala hilo.
Alisema kwa kuzingatia suala hilo imeanza operesheni ya kukamata watu wanaodurufu kazi za wasanii na kuziuza mitaani kwa bei nafuu ambazo hazina stampu ili kukomesha tatizo hilo.
Alisema kazi za wasanii zimekuwa zikidurufiwa sana na kuuzwa mitaani kwa bei nafuu na kuacha kununua CD ambazo zimethibitishwa na Cosota na kupewa hatimiliki ambazo zinatambulika kisheria na kubandikwa stampu na mamlaka hiyo.
Alisema kuwa tayari wameshakamata mitambo mbalimbali ambayo inatumika kudurufu kazi hizo maeneo ya Kariakoo na watu wanaoziuza na kuwachukulia hatua ili waweze kumaliza tatizo hilo.
Hata hivyo alisema msanii yeyote lazima apitie Basata na Cosota ili aweze kupewa hati miliki baada ya hapo anapeleka kazi zake TRA ili ziweze kuwekwa stampu ambazo zitakuwa halali kuuzwa sokoni.
Pia alisema wameshaunda timu ambayo imehusisha watu kutoka TRA, Cosota na Basata ambao wanafanya operesheni hiyo katika maeneo mbalimbali ili kubaini watu wanaouza CD ambazo hazina stampu kwani hali hiyo inakosesha wasanii wengi mapato.
Aidha, imesema TRA inataka kuboresha mfumo wa utoaji stampu ziwe za kielektroniki na kuachana na za karatasi ili ziwe bora zaidi katika bidhaa zote.
Hayo yalibainishwa Dar es Salaam jana na Mkurugenzi wa tafiti na sera wa (TRA), Tonedeus Muganyizi katika Maonesho ya 38 ya Biashara Kimataifa yanayofanyika katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere katika barabara ya Kilwa maarufu kama Sabasaba.
Alisema mwitikio wa wasanii bado uko chini hasa wasanii wa muziki katika kupambana na watu hao kwani hawajawa na mwamko wa kuweka kazi zao stampu lakini wasanii wakubwa wa filamu wamekuwa na mwamko na uelewa juu ya suala hilo.
Alisema kwa kuzingatia suala hilo imeanza operesheni ya kukamata watu wanaodurufu kazi za wasanii na kuziuza mitaani kwa bei nafuu ambazo hazina stampu ili kukomesha tatizo hilo.
Alisema kazi za wasanii zimekuwa zikidurufiwa sana na kuuzwa mitaani kwa bei nafuu na kuacha kununua CD ambazo zimethibitishwa na Cosota na kupewa hatimiliki ambazo zinatambulika kisheria na kubandikwa stampu na mamlaka hiyo.
Alisema kuwa tayari wameshakamata mitambo mbalimbali ambayo inatumika kudurufu kazi hizo maeneo ya Kariakoo na watu wanaoziuza na kuwachukulia hatua ili waweze kumaliza tatizo hilo.
Hata hivyo alisema msanii yeyote lazima apitie Basata na Cosota ili aweze kupewa hati miliki baada ya hapo anapeleka kazi zake TRA ili ziweze kuwekwa stampu ambazo zitakuwa halali kuuzwa sokoni.
Pia alisema wameshaunda timu ambayo imehusisha watu kutoka TRA, Cosota na Basata ambao wanafanya operesheni hiyo katika maeneo mbalimbali ili kubaini watu wanaouza CD ambazo hazina stampu kwani hali hiyo inakosesha wasanii wengi mapato.