Idara ya Uhamiaji imewataka wananchi kutoa taarifa pale wanapoona kuna wahamiaji haramu wanaishi katika mazingira yao au wanaishi bila kibali hapa nchini ili wachukuliwe hatua.
Ofisa Uhusiano wa Idara ya Uhamiaji, Tatu Burhani,alisema hayo jana katika Maonesho ya 38 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam, yanayofanyika katika barabara ya Kilwa katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere maarufu kama Sabasaba.
Alisema kuwa wananchi wanatakiwa kutoa taarifa za wageni wanaowaona katika maeneo yao ya makazi au waliowatilia shaka ili kubaini kama wapo kisheria hapa nchini.
"Kuna wageni mbalimbali wanaingia hapa nchini kupitia barabara za panya hivyo ni vyema wananchi wakashirikiana na Uhamiaji ili kuwafichua na sheria ichukue mkondo wake,"alisema Burhani.
Pia alisema kuna baadhi ya wageni wanaoingia hapa nchini kihalali kwa lengo la kutembea lakini baada ya muda utawakuta anafanya kazi sehemu hao ni wahamiaji haramu kwani kibali alichopewa ni cha kutembea tu hivyo wananchi wakibaini watu kama hao watoe taarifa.
Hata hivyo alisema kuwa wanakabiliwa na changamoto mbalimbali moja ikiwa ni ukubwa wa mipaka ya Tanzania hivyo kushindwa kuwadhibiti maeneo yote kutokana na wageni wengine hupitia njia za panya kuingia nchini.
Pia alisema wanakabiliwa na changamoto za kijamii kama zinazotokana na mwingiliano wa watu kutoka sehemu moja kwenda nyingine katika nchi tunazopakana nazo.
Alisema kutoka na hali hiyo wamejipanga kuimarisha doria, misako na oparesheni mbalimbali ili kuwasaka wahamiji haramu wanaoishi hapa nchini kinyume na taratibu.
Pia alisema wanaongeza mafunzo kwa watumishi wa idara hiyo ili kubaini mbinu mbalimbali wanazotumia wahamiaji haramu kuingia hapa nchini.
Ofisa Uhusiano wa Idara ya Uhamiaji, Tatu Burhani,alisema hayo jana katika Maonesho ya 38 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam, yanayofanyika katika barabara ya Kilwa katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere maarufu kama Sabasaba.
Alisema kuwa wananchi wanatakiwa kutoa taarifa za wageni wanaowaona katika maeneo yao ya makazi au waliowatilia shaka ili kubaini kama wapo kisheria hapa nchini.
"Kuna wageni mbalimbali wanaingia hapa nchini kupitia barabara za panya hivyo ni vyema wananchi wakashirikiana na Uhamiaji ili kuwafichua na sheria ichukue mkondo wake,"alisema Burhani.
Pia alisema kuna baadhi ya wageni wanaoingia hapa nchini kihalali kwa lengo la kutembea lakini baada ya muda utawakuta anafanya kazi sehemu hao ni wahamiaji haramu kwani kibali alichopewa ni cha kutembea tu hivyo wananchi wakibaini watu kama hao watoe taarifa.
Hata hivyo alisema kuwa wanakabiliwa na changamoto mbalimbali moja ikiwa ni ukubwa wa mipaka ya Tanzania hivyo kushindwa kuwadhibiti maeneo yote kutokana na wageni wengine hupitia njia za panya kuingia nchini.
Pia alisema wanakabiliwa na changamoto za kijamii kama zinazotokana na mwingiliano wa watu kutoka sehemu moja kwenda nyingine katika nchi tunazopakana nazo.
Alisema kutoka na hali hiyo wamejipanga kuimarisha doria, misako na oparesheni mbalimbali ili kuwasaka wahamiji haramu wanaoishi hapa nchini kinyume na taratibu.
Pia alisema wanaongeza mafunzo kwa watumishi wa idara hiyo ili kubaini mbinu mbalimbali wanazotumia wahamiaji haramu kuingia hapa nchini.