Wakulima wa zao la pamba na wanunuzi wa zao hilo, wamekuwa ni chanzo cha kudhoofisha zao hilo, hivyo kushindwa kuingia katika ushindani wa soko.
Imedaiwa kuwa baadhi ya wakulima wamekuwa wakiweka maji kwenye pamba, ili kuongeza uzito wa pamba, hasa pale inapotangazwa bei ndogo ya pamba.
Pia, imedaiwa kuwa wanunuzi na wahasibu, nao hunyunyizia chumvi au sukari, kwa lengo la kuongeza uzito wa pamba ili kupata faida.
Hayo yalisemwa na baadhi ya wadau wa zao hilo kutoka wilaya za Bariadi na Itilima mkoani Simiyu.
Walisema hayo katika mdahalo, ulioandaliwa na shirika lisilo la kiserikali lenye kutetea masuala ya utawala bora, uwajibikaji na kilimo la ADLG, kwa ufadhili wa Jukwaa la mashirika yanayojihusisha na kilimo (ANSAF).
Mmoja wa wadau hao kutoka wilayani Bariadi, Moses Sosoma alisema pamba inalimwa Bariadi, sio kwa lengo la kibiashara, bali linalimwa ili kuondoa changamoto ndogo kwenye kaya.
Pia, alisema baadhi ya wakulima katika wilaya hiyo, wamekuwa wakidiriki kuchanganya pamba na maji, chumvi na sukari kwa lengo kuongeza uzito. Alisema vitendo hivyo vimefanya zao hilo, kukosa thamani.
“Kila msimu wakulima wamekuwa wakilalamikia ubora wa pamba kutokana na kushuka kwa bei. Kinachotakiwa kwa sasa ni wakulima waandaliwe kuanzia ngazi ya chini kwa kuelimishwa ubora unaotakiwa ili kupata bei nzuri?” alisema Diwani wa Kata ya Bariadi, David Sendo.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi, Bahati Magamula alisema kumekuwepo na changamoto nyingi kwenye kilimo cha zao la pamba katika mkoa wa Simiyu, unaoongoza kwa uzalishaji wa zao hilo nchini. Alisema mkoa huo unazalisha asilimia 40 ya pamba yote inayolimwa nchini.
Alisema hakuna ufumbuzi uliopatikana hadi sasa, kuhusu changamoto za zao hilo Alisema kila mwaka wamekuwa wakikaa vikao vingi, lakini wameshindwa kupata majibu huku wakulima wakizidi kuumia.
Mtafiti wa Kujitegemea wa zao la pamba, Geofrey Chambua alisema kuanzia mwaka 2005 hadi 2009, uzalishaji wa zao wa pamba ulikuwa mkubwa na liliweza kuingiza Taifa Sh bilioni 92, hivyo kuwa zao la kwanza katika kuingiza pato kubwa.
Lakini, baada ya hapo, uzalishaji umeendelea kushuka, ambapo katika musimu wa mwaka 2012/13, zilizalishwa tani 351,151 na mwaka 2013/14 uzalishaji ulikuwa tani 246,767.
“Kushuka kwa bei ya pamba, kulitokana na kuvurugika kwa mfumo msimu uliopita, ambapo bei ilikuwa shilingi 700 kwa kilo na sasa ni shilingi 750. Kinachochangia bei hiyo ni kukosekana kwa viwanda vya ndani, ambavyo vingeleta ushindani katika soko. Kule Marekani pamba yake ipo kwenye ushindani, kwa sababu nchi hiyo ina viwanda vingi. Pamba ya Tanzania ni ya mwisho duniani katika soko,” alisema Chambua.
Mkurugenzi wa shirika hilo, Jimmy Luhende alisema pamba inayotoka shambani ni safi na inavunwa kwa kutumia mkono.
Alisema changamoto kubwa zilizojitokeza ni gharama kubwa za uzalishaji, wakati kipato cha wakulima, wanachotumia katika kilimo hicho, ni kidogo.
Alitaja changamoto zingine kuwa ni mbegu zinapopandwa kutochipua vizuri na baadhi ya dawa za kuua wadudu kuwa feki.
Imedaiwa kuwa baadhi ya wakulima wamekuwa wakiweka maji kwenye pamba, ili kuongeza uzito wa pamba, hasa pale inapotangazwa bei ndogo ya pamba.
Pia, imedaiwa kuwa wanunuzi na wahasibu, nao hunyunyizia chumvi au sukari, kwa lengo la kuongeza uzito wa pamba ili kupata faida.
Hayo yalisemwa na baadhi ya wadau wa zao hilo kutoka wilaya za Bariadi na Itilima mkoani Simiyu.
Walisema hayo katika mdahalo, ulioandaliwa na shirika lisilo la kiserikali lenye kutetea masuala ya utawala bora, uwajibikaji na kilimo la ADLG, kwa ufadhili wa Jukwaa la mashirika yanayojihusisha na kilimo (ANSAF).
Mmoja wa wadau hao kutoka wilayani Bariadi, Moses Sosoma alisema pamba inalimwa Bariadi, sio kwa lengo la kibiashara, bali linalimwa ili kuondoa changamoto ndogo kwenye kaya.
Pia, alisema baadhi ya wakulima katika wilaya hiyo, wamekuwa wakidiriki kuchanganya pamba na maji, chumvi na sukari kwa lengo kuongeza uzito. Alisema vitendo hivyo vimefanya zao hilo, kukosa thamani.
“Kila msimu wakulima wamekuwa wakilalamikia ubora wa pamba kutokana na kushuka kwa bei. Kinachotakiwa kwa sasa ni wakulima waandaliwe kuanzia ngazi ya chini kwa kuelimishwa ubora unaotakiwa ili kupata bei nzuri?” alisema Diwani wa Kata ya Bariadi, David Sendo.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi, Bahati Magamula alisema kumekuwepo na changamoto nyingi kwenye kilimo cha zao la pamba katika mkoa wa Simiyu, unaoongoza kwa uzalishaji wa zao hilo nchini. Alisema mkoa huo unazalisha asilimia 40 ya pamba yote inayolimwa nchini.
Alisema hakuna ufumbuzi uliopatikana hadi sasa, kuhusu changamoto za zao hilo Alisema kila mwaka wamekuwa wakikaa vikao vingi, lakini wameshindwa kupata majibu huku wakulima wakizidi kuumia.
Mtafiti wa Kujitegemea wa zao la pamba, Geofrey Chambua alisema kuanzia mwaka 2005 hadi 2009, uzalishaji wa zao wa pamba ulikuwa mkubwa na liliweza kuingiza Taifa Sh bilioni 92, hivyo kuwa zao la kwanza katika kuingiza pato kubwa.
Lakini, baada ya hapo, uzalishaji umeendelea kushuka, ambapo katika musimu wa mwaka 2012/13, zilizalishwa tani 351,151 na mwaka 2013/14 uzalishaji ulikuwa tani 246,767.
“Kushuka kwa bei ya pamba, kulitokana na kuvurugika kwa mfumo msimu uliopita, ambapo bei ilikuwa shilingi 700 kwa kilo na sasa ni shilingi 750. Kinachochangia bei hiyo ni kukosekana kwa viwanda vya ndani, ambavyo vingeleta ushindani katika soko. Kule Marekani pamba yake ipo kwenye ushindani, kwa sababu nchi hiyo ina viwanda vingi. Pamba ya Tanzania ni ya mwisho duniani katika soko,” alisema Chambua.
Mkurugenzi wa shirika hilo, Jimmy Luhende alisema pamba inayotoka shambani ni safi na inavunwa kwa kutumia mkono.
Alisema changamoto kubwa zilizojitokeza ni gharama kubwa za uzalishaji, wakati kipato cha wakulima, wanachotumia katika kilimo hicho, ni kidogo.
Alitaja changamoto zingine kuwa ni mbegu zinapopandwa kutochipua vizuri na baadhi ya dawa za kuua wadudu kuwa feki.