Quantcast
Channel: ziro99blog
Viewing all articles
Browse latest Browse all 4500

WAJAWAZITO WASIOONGOZANA NA WENZA WANYIMWA MATIBABU KLINIKI

$
0
0

Idadi kubwa ya wajawazito katika Tarafa  ya Mwese, Halmashauri ya Wilaya  ya  Mpanda  mkoani Katavi,  wanalazimika  kutohudhuria kliniki na kujifungulia  nyumbani, kwa madai ya kukataliwa kuhudumiwa katika  kliniki  ya eneo  hilo, wanapokwenda bila ya wenza wao.
Inadaiwa kuwa wanaume wengi  katika Tarafa  hiyo ya Mwese,  wanakataa kuwasindikiza kliniki wenza  wao  kwa hofu kuwa  watalazimishwa kupima  afya zao,  hususani Maambukizi  ya Virusi vya Ukimwi (VVU).
Diwani  wa Viti Maalumu  wa Kata  ya Mwese, Theodola Kisesa  alibainisha hayo  wakati akichangia  katika Kikao  cha Baraza la Madiwani  wa Halmshauri ya Wilaya ya Mpanda  kilichoketi juzi mjini hapa.
Akifafanua, alisema wajawazito katika tarafa  hiyo wamekuwa wakikataliwa kupimwa afya zao  na watoa  huduma  katika kliniki,  wanaposhindwa kuongozana na  wenza  wao wa kiume  ili  nao  waweze kupima afya zao.
“Watoa huduma katika kliniki  hii  ya Tarafa ya Mwese  wanawataka wajawazito  kuandamana  na  wenza wao  ili nao  waweze  kupima  afya zao  katika jitihada za  kuzuia  maambukizi  ya VVU  kutoka kwa mama na mtoto… sasa  wanaume wengi  wamekuwa  wanasita.
“Hivyo  baada ya kukataliwa  wajawazito wengi  wamekuwa  wakilazimika kujifungulia  nyumbani  au kwa wakunga wa jadi  ambao  hawana ujuzi  wa kutosha  hivyo  kusababisha maisha ya mama  na mtoto  ambaye  hajazaliwa kuwa mashakani, “ alisisitiza.
Mganga Mkuu wa Wilaya ya Mpanda, Dk Joseph Msemwa akichangia  alisisitiza kuwa jukumu la kupimwa afya, sio la mama peke yake, bali  kwa  wenza wote.
Alisema anazo  taarifa kuwa mama akipimwa na kugundulika hana maambukizi ya VVU, mwenza  wake  anaamini naye yuko salama, jambo alilosisitiza kuwa halina ukweli.
Aidha, aliagiza wajawazito wahudumiwe katika vituo vya kutolea huduma bila  ya ubaguzi, hata kwa ambao hawakuongozana na wenza  wao.

Viewing all articles
Browse latest Browse all 4500

Trending Articles