Mkazi wa mtaa wa Nsemulwa, Athuman Mussa (54) amehukumiwa kifungo cha maisha jela na Mahakama ya Wilaya ya Mpanda, baada ya kutiwa hatiani kwa kosa la kumnajisi mtoto wa kike mwenye umri wa miaka minne mdomoni.
Hukumu hiyo ilitolewa juzi na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa mahakama hiyo, Chiganga Ntegwa baada ya kuridhishwa na ushahidi uliotolewa mahakamani hapo na upande wa mashitaka uliongozwa na Mwendesha Mashtaka, Mkaguzi wa Polisi, Ally Mbwijo.
Kwa mujibu wa hati ya mashtaka, mshtakiwa anadaiwa kutenda kosa hilo Juni 26 mwaka jana saa 12:00 jioni nyumbani kwake katika mtaa wa Nsemulwa katika Mji wa Mpanda.
Akisoma hukumu hiyo, Hakimu Ntengwa alieleza kuwa siku hiyo ya tukio mshitakiwa alimkuta mtoto huyo ambaye wazazi wake ni jirani zake akiwa anacheza na watoto wenzake karibu na nyumba yake akamwita na kuingia naye ndani akiahidi kumpatia zawadi ya pipi aina ya jojo.
Baada ya mtoto huyo kuingia ndani ya nyumba, Athumani alimvuta kwenye kochi sebuleni na kisha alimwingizia uume wake kwenye mdomo wa mtoto huyo hadi hapo alipomaliza haja yake kisha akamwamuru aondoke nyumbani kwake ndipo mtoto huyo alipotoka mbio na kurejea kwao akilia.
Aliiambia mahakama baada ya mtoto huyo kufika nyumbani kwao mama yake alimuuliza kilichomfanya alie ndipo alitema mbegu za kiume ambazo zilikuwa mdomoni mwake na kisha alimwelezea mama yake kila kitu alichotendewa na mshitakiwa.
Baada ya mama kuelezwa unyama huo aliofanyiwa mtoto wake, naye alianza kulia kwa nguvu na kusababisha majirani kufika nyumbani hapo ambapo walielezwa alichofanyiwa mtoto huyo ndipo majirani walikwenda nyumbani kwa mshitakiwa wakamkamata na kumfikisha kwenye kituo cha polisi.
Ntengwa alieleza mahakamani hapo kuwa mahakama baada ya kusikiliza mwenendo mzima wa kesi kwa pande zote mbili za mashitaka na utetezi, mahakama imemwona mshitakiwa amepatikana na hatia hivyo kabla ya mahakama haijamwadhibu ilimpatia nafasi ya mshitakiwa kusema jambo au kama ana sababu za msingi aombe kupunguziwa adhabu.
Mshitakiwa aliiomba mahakama imwachie huru kwani hakufanya kitendo hicho na zile mbegu za kiume alizotema mtoto huyo zilikuwa ni karanga alizokuwa akila mtoto huyo.
Mwendesha mashitaka, Mbwijo alipinga utetezi huo na kuiomba mahakama itoe adhabu kali kwa mshitakiwa ili iwe fundisho kwa watu wengine wenye tabia kama hiyo.
Hukumu hiyo ilitolewa juzi na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa mahakama hiyo, Chiganga Ntegwa baada ya kuridhishwa na ushahidi uliotolewa mahakamani hapo na upande wa mashitaka uliongozwa na Mwendesha Mashtaka, Mkaguzi wa Polisi, Ally Mbwijo.
Kwa mujibu wa hati ya mashtaka, mshtakiwa anadaiwa kutenda kosa hilo Juni 26 mwaka jana saa 12:00 jioni nyumbani kwake katika mtaa wa Nsemulwa katika Mji wa Mpanda.
Akisoma hukumu hiyo, Hakimu Ntengwa alieleza kuwa siku hiyo ya tukio mshitakiwa alimkuta mtoto huyo ambaye wazazi wake ni jirani zake akiwa anacheza na watoto wenzake karibu na nyumba yake akamwita na kuingia naye ndani akiahidi kumpatia zawadi ya pipi aina ya jojo.
Baada ya mtoto huyo kuingia ndani ya nyumba, Athumani alimvuta kwenye kochi sebuleni na kisha alimwingizia uume wake kwenye mdomo wa mtoto huyo hadi hapo alipomaliza haja yake kisha akamwamuru aondoke nyumbani kwake ndipo mtoto huyo alipotoka mbio na kurejea kwao akilia.
Aliiambia mahakama baada ya mtoto huyo kufika nyumbani kwao mama yake alimuuliza kilichomfanya alie ndipo alitema mbegu za kiume ambazo zilikuwa mdomoni mwake na kisha alimwelezea mama yake kila kitu alichotendewa na mshitakiwa.
Baada ya mama kuelezwa unyama huo aliofanyiwa mtoto wake, naye alianza kulia kwa nguvu na kusababisha majirani kufika nyumbani hapo ambapo walielezwa alichofanyiwa mtoto huyo ndipo majirani walikwenda nyumbani kwa mshitakiwa wakamkamata na kumfikisha kwenye kituo cha polisi.
Ntengwa alieleza mahakamani hapo kuwa mahakama baada ya kusikiliza mwenendo mzima wa kesi kwa pande zote mbili za mashitaka na utetezi, mahakama imemwona mshitakiwa amepatikana na hatia hivyo kabla ya mahakama haijamwadhibu ilimpatia nafasi ya mshitakiwa kusema jambo au kama ana sababu za msingi aombe kupunguziwa adhabu.
Mshitakiwa aliiomba mahakama imwachie huru kwani hakufanya kitendo hicho na zile mbegu za kiume alizotema mtoto huyo zilikuwa ni karanga alizokuwa akila mtoto huyo.
Mwendesha mashitaka, Mbwijo alipinga utetezi huo na kuiomba mahakama itoe adhabu kali kwa mshitakiwa ili iwe fundisho kwa watu wengine wenye tabia kama hiyo.