Quantcast
Channel: ziro99blog
Viewing all articles
Browse latest Browse all 4621

WIVU WA MAPENZI, UROHO WA MALI WASABABISHA MAAFA RUKWA

$
0
0
Watu watano wamekufa mkoani Rukwa katika matukio tofauti, akiwemo Silvia Patrick aliyeuawa na mumewe kwa kuchomwa kisu kifuani kutokana na wivu wa mapenzi.
Joseph Dominick (33) baada ya kumuua mkewe huyo mwenye miaka 26, alijaribu kujiua kwa kujichoma kisu tumboni, lakini hakufa na amelazwa katika Kituo cha Afya cha Kamasamba wilayani Momba mkoani Mbeya akiwa chini ya ulinzi.
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, Frednand Rwegasira  alisema mtuhumiwa alitenda uhalifu huo  juzi saa 4:00 usiku  akiwa nyumbani kwake kijijini Kawila na chanzo kikielezwa kuwa  wivu wa mapenzi  uliochanganyika na ulevi  wa pombe.
“Mkewe alikufa papo hapo  baada ya kuchomwa  kisu  kifuani  ndipo mtuhumiwa  naye aliamua kujichoma na kisu tumboni  akijaribu kujiua  lakini aliokolewa na  majirani  na kukimbizwa katika Kituo cha Afya  alikolazwa kwa matibabu,” alieleza.
Katika tukio lingine,  mkazi  wa kijiji cha Kalaembe wilayani Kalambo, Braza Simfukwe (43)  ameuawa baada ya kushambuliwa kwa  kuchomwa kisu  tumboni na wadogo zake  watatu wa tumbo moja  wakigombea  mali za urithi  zilizoachwa na  marehemu  baba yao.
Kaimu Kamanda Rwegasira amewataja  ndugu  hao watatu  waliotenda uhalifu huo kuwa ni pamoja na Mogani Simfukwe, Gervas Simfukwe na Kilani Simfukwe ambao  wote walitoroka baada ya kutenda  uhalifu huo  na sasa  wanasakwa  na Polisi.
Kwa mujibu  wa Kaimu Kamanda, uchunguzi  wa awali  umebaini kuwa  baada ya  baba yao  kufariki dunia mwaka jana, Braza  alianza kumiliki  mali  zake alizoziacha  ikiwemo  nyumba na mashamba,  kitendo  kilichowachukiza  wadogo zake  na kusababisha mgogoro mkubwa baina  yao.
Inadaiwa Braza alifuatwa na wadogo zake hao  watatu  wenye hasira  akiwa nyumbani kwake kijijini  humo na kumshambulia  kwa  visu  ambapo  alifikwa na mauti katika Kituo cha Afya cha Matai  alikolazwa kwa matibabu.
Kwa mujibu  wa Kaimu Kamanda huyo, mkazi  wa kitongoji cha Bangwe, Manispaa ya Sumbawanga, Malyatanga Mwami (42) alikufa baada ya kuanguka ghafla akiwa njiani kurejea kwake akitoka  kunywa pombe za kienyeji  kilabuni.
“Uchunguzi wa kitabibu  umebaini kuwa Mwami  alikunywa pombe  kwa muda mrefu  bila kula …. uchunguzi zaidi wa mkasa  huo bado unaendelea," alieleza Rwegasira.
Katika  hatua  nyingine, Rwegasira alibainisha kuwa  mtu mmoja amekufa  wilayani Sumbawanga  katika ajali ya barabarani  iliyotokea  saa 1:00, juzi  kijijini Miangalua  katika  barabara ya Sumbawanga – Mbeya.
Inadaiwa  ajali hiyo ya  barabarani  ilihusisha  gari aina ya TATA yenye  namba za usajili  T 568 ATR  lililokuwa likiendeshwa na Andrew Mwandembwa (30) mkazi wa  eneo  la Soweto,  Jijini Mbeya  lililogongana na pikipiki aina ya T/BETTER yenye namba za usajili T 211 CVD.
Alitamja marehemu kuwa ni Derick Tano 'Laiton' (24) , mkazi wa  kijiji cha  Miangalua kwamba uchaguzi wa awali umebainisha kuwa  chanzo  cha ajali hiyo  ni mwendo kasi wa pikipiki ambapo dereva wa  gari  amekamatwa na atafikishwa  mahakamani mara uchunguzi  wa awali  utakapokamilika.
Rwegasira  amebainisha kuwa mkazi  wa eneo la Katandala, Manispaa ya Sumbawanga aliyefahamika kwa jina moja la Manson  anayekadiriwa  kuwa na umri wa miaka 25 ameuawa  na kundi  la  wananchi wakimtuhumu kuwa  mwizi. Hakuna yeyote aliyekamatwa  kuhusu  mauaji hayo  na uchunguzi zaidi unaendelea.

Viewing all articles
Browse latest Browse all 4621

Trending Articles