Rais Jakaya Kikwete anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika kilele cha maadhimisho ya Jubilei ya miaka 75 ya Kanisa la Tanzania Assemblies of God (TAG), yatakayofanyika Jumapili ijayo kwenye Uwanja wa Michezo wa Sokoine jijini Mbeya.
Hayo yamethibitishwa na Askofu Mkuu wa Kanisa la TAG nchini, Askofu Barnabas Mtokambali katika hotuba yake iliyosomwa juzi na Askofu wa Jimbo la Rukwa, Askofu Aron Shimwela.
Alisema hayo katika hafla ya ugawaji wa shuka 1,300 zilizotolewa na kanisa hilo. Hafla hiyo ilifanyika katika Hospitali ya Mkoa wa Rukwa mjini hapa.
Akifafanua, alisema tangu kuanza kwa maadhimisho ya Jubilei ya miaka 75 ya Kanisa la TAG, kanisa limekuwa likifanya shughuli mbalimbali, ikiwemo huduma kwa jamii, ikiwa ni pamoja na kufanya usafi katika maeneo mbalimbali.
Pia wamekuwa wakitembelea na kutoa misaada mbalimbali katika magereza, vituo vya kulelea watoto yatima, hospitali, zahanati na vituo vya afya, ikiwa ni pamoja na kuchangia damu katika hospitali mbalimbali.
Askofu Shimwela alisema kuanzia Julai mosi hadi Julai 4 mwaka huu, Kanisa la TAG limegawa vyandarua katika hospitali na vituo vyote vya afya vinavyomilikiwa na Serikali, taasisi za dini na binafsi katika mikoa ya Mbeya, Rukwa na Njombe.
“Vyandarua takribani 8,550 vimegawiwa katika hospitali 34 na vituo vya afya 83 katika mikoa ya Rukwa, Mbeya na Njombe …Kanisa la TAG kama sehemu ya jamii linatambua ukubwa wa tatizo la ugonjwa wa malaria hasa kwa wajawazito na watoto chini ya miaka mitano
“Hivyo pamoja na kutoa huduma ya kiroho pia tunaunga mkono jitihada za Serikali katika kufikia Malengo ya Milenia katika mapambano dhidi ya malaria,“ alisema Askofu Shimwela.
Katika ghafla hiyo ya makabidhiano, Askofu Shimwela kwa niaba ya Askofu Mkuu wa TAG, alimkabidhi Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Dk Emmanuel Mtika vyandarua 1,300 vitakavyogawiwa katika hospitali tatu na vituo vya afya 22 mkoani humo na zahanati zinazolaza wagonjwa.
Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga, Mathew Sedoyeka alilishukuru kanisa hilo kwa msaada huo. Pia, alimtaka Mganga Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, kuhakikisha kuwa msaada huo unatumika kwa malengo yaliyokusudiwa na si vinginevyo.
Hayo yamethibitishwa na Askofu Mkuu wa Kanisa la TAG nchini, Askofu Barnabas Mtokambali katika hotuba yake iliyosomwa juzi na Askofu wa Jimbo la Rukwa, Askofu Aron Shimwela.
Alisema hayo katika hafla ya ugawaji wa shuka 1,300 zilizotolewa na kanisa hilo. Hafla hiyo ilifanyika katika Hospitali ya Mkoa wa Rukwa mjini hapa.
Akifafanua, alisema tangu kuanza kwa maadhimisho ya Jubilei ya miaka 75 ya Kanisa la TAG, kanisa limekuwa likifanya shughuli mbalimbali, ikiwemo huduma kwa jamii, ikiwa ni pamoja na kufanya usafi katika maeneo mbalimbali.
Pia wamekuwa wakitembelea na kutoa misaada mbalimbali katika magereza, vituo vya kulelea watoto yatima, hospitali, zahanati na vituo vya afya, ikiwa ni pamoja na kuchangia damu katika hospitali mbalimbali.
Askofu Shimwela alisema kuanzia Julai mosi hadi Julai 4 mwaka huu, Kanisa la TAG limegawa vyandarua katika hospitali na vituo vyote vya afya vinavyomilikiwa na Serikali, taasisi za dini na binafsi katika mikoa ya Mbeya, Rukwa na Njombe.
“Vyandarua takribani 8,550 vimegawiwa katika hospitali 34 na vituo vya afya 83 katika mikoa ya Rukwa, Mbeya na Njombe …Kanisa la TAG kama sehemu ya jamii linatambua ukubwa wa tatizo la ugonjwa wa malaria hasa kwa wajawazito na watoto chini ya miaka mitano
“Hivyo pamoja na kutoa huduma ya kiroho pia tunaunga mkono jitihada za Serikali katika kufikia Malengo ya Milenia katika mapambano dhidi ya malaria,“ alisema Askofu Shimwela.
Katika ghafla hiyo ya makabidhiano, Askofu Shimwela kwa niaba ya Askofu Mkuu wa TAG, alimkabidhi Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Dk Emmanuel Mtika vyandarua 1,300 vitakavyogawiwa katika hospitali tatu na vituo vya afya 22 mkoani humo na zahanati zinazolaza wagonjwa.
Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga, Mathew Sedoyeka alilishukuru kanisa hilo kwa msaada huo. Pia, alimtaka Mganga Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, kuhakikisha kuwa msaada huo unatumika kwa malengo yaliyokusudiwa na si vinginevyo.