Kampuni ya Strabag International GmbH inayojenga barabara kwa ajili ya mabasi yaendayo haraka mjini Dar es Salaam, imetangaza kufunga barabara ya Kawawa/ Morocco kesho na keshokutwa ili kupisha ujenzi.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana, imesema watumiaji wa barabara ya Kinondoni kuelekea Morocco na Magomeni wanashauriwa kutumia barabara ya Togo kupitia Karago kama njia mbadala.
Aidha wale wanaotokea Morocco au Kawawa kuelekea Kinondoni Makaburini wanashauriwa kutumia barabara ya Mtama.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana, imesema watumiaji wa barabara ya Kinondoni kuelekea Morocco na Magomeni wanashauriwa kutumia barabara ya Togo kupitia Karago kama njia mbadala.
Aidha wale wanaotokea Morocco au Kawawa kuelekea Kinondoni Makaburini wanashauriwa kutumia barabara ya Mtama.