![]() |
Dk Rajab Rutengwe. |
Mkuu wa Mkoa wa Katavi , Dk Rajab Rutengwe ametoa ushuhuda wake jinsi alivyoponea chupuchupu, kuhadaiwa na mkazi mmoja mjini Mpanda jana asubuhi, ambayo ilikuwa Siku ya Wajinga Duniani.
Dk Rutengwe alitoa ushuhuda wake mbele wa wadau wa kikao, kilichowakutanisha kujadili sheria ndogo za uanzishwaji wa Mfuko wa Bima ya Afya (CHF) na Tiba kwa Kadi (TIKA) kilichofanyika leo mjini hapa.
wadau wa kikao kilichokutanisha kujadili sheria ndogo za uanzishwaji wa Mfuko wa Bima ya Afya (CHF) na Tiba kwa Kadi (TIKA) kilichofanyika leo mjini hapa.
“Leo (jana) asubuhi nusura niingizwe mjini, kwani nilikuwa sina habari kuwa ni Siku ya Wajinga Duniani, nilipokea simu ya mtu mmoja ambaye hakujitaja jina, akaniomba msaada eti alikuwa ameunguliwa na nyumba yake na kupata hasara kubwa ya vitu vyake vya thamani kuteketea kwa moto,” alisema.
Aliendelea kusema, “lakini baada ya kufikiria kwa kina na kujiuliza mbona Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa pia ya Wilaya hazijanipa ripoti, ndipo baadaye nikabaini kuwa leo (jana) ilikuwa ni Siku ya Wajinga Duniani.”
Awali, akimkaribisha mgeni rasmi, Mkuu wa Wilaya ya Mpanda, Paza Mwamlima aliguswa na mahudhurio makubwa ya wakuu wa idara.
“ Nimeguswa sana na mahudhurio makubwa, hususani ya watendaji wenu, ambao mara nyingi hawahudhurii vikao vyetu, ambavyo havina posho sasa baada ya kusikia kuwa kikao hiki inatolewa posho wamehudhuria kwa wingi,” alisema Mwamlima.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bima ya Taifa ya Afya (NHIF), Celestine Mugongo alisema halmashauri zipatazo 40 katika mikoa mbalimbali nchini, zitaunganishwa katika mpango wa huduma ya Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF), ikiwa ni mkakati wa NHIF kuhakikisha kila mwananchi anapata huduma bora za matibabu.
Dk Rutengwe alitoa ushuhuda wake mbele wa wadau wa kikao, kilichowakutanisha kujadili sheria ndogo za uanzishwaji wa Mfuko wa Bima ya Afya (CHF) na Tiba kwa Kadi (TIKA) kilichofanyika leo mjini hapa.
wadau wa kikao kilichokutanisha kujadili sheria ndogo za uanzishwaji wa Mfuko wa Bima ya Afya (CHF) na Tiba kwa Kadi (TIKA) kilichofanyika leo mjini hapa.
“Leo (jana) asubuhi nusura niingizwe mjini, kwani nilikuwa sina habari kuwa ni Siku ya Wajinga Duniani, nilipokea simu ya mtu mmoja ambaye hakujitaja jina, akaniomba msaada eti alikuwa ameunguliwa na nyumba yake na kupata hasara kubwa ya vitu vyake vya thamani kuteketea kwa moto,” alisema.
Aliendelea kusema, “lakini baada ya kufikiria kwa kina na kujiuliza mbona Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa pia ya Wilaya hazijanipa ripoti, ndipo baadaye nikabaini kuwa leo (jana) ilikuwa ni Siku ya Wajinga Duniani.”
Awali, akimkaribisha mgeni rasmi, Mkuu wa Wilaya ya Mpanda, Paza Mwamlima aliguswa na mahudhurio makubwa ya wakuu wa idara.
“ Nimeguswa sana na mahudhurio makubwa, hususani ya watendaji wenu, ambao mara nyingi hawahudhurii vikao vyetu, ambavyo havina posho sasa baada ya kusikia kuwa kikao hiki inatolewa posho wamehudhuria kwa wingi,” alisema Mwamlima.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bima ya Taifa ya Afya (NHIF), Celestine Mugongo alisema halmashauri zipatazo 40 katika mikoa mbalimbali nchini, zitaunganishwa katika mpango wa huduma ya Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF), ikiwa ni mkakati wa NHIF kuhakikisha kila mwananchi anapata huduma bora za matibabu.