Jamaa watatu walikamatwa na bangi huko China. Wakapewa adhabu ya kwenda msituni na kurejea na matunda kumi kila mmoja. Wa kwanza akarejea na machungwa. Akaambiwa ameze moja-moja, akashindwa na kupigwa risasi. Wa pili akarejea na nyanya chungu. Naye akaambiwa ameze moja-moja, alipofika ya tisa akaacha na kuanza kucheka hivyo akapigwa risasi. Wakiwa kuzimu, jamaa wa kwanza akamuuliza wa kwanza kwanini aliamua kucheka. Jamaa wa pili akajibu: "Nilipogeuka nyuma nikamwona jamaa wa tatu karejea na matikiti-maji!" Balaa...
↧