Mkazi wa kijiji cha Fyengelezya, Manispaa ya Sumbawanga, Didas Choma (35), ameuawa kikatili na mdogo wake wa tumbo moja, Frank Choma (30), kwa kumkata kichwa kwa shoka kutokana na mgogoro wa shamba la urithi.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, Jacob Mwaruanda, amethibitisha kutokea kwa mauaji hayo ya kikatili kijijini Fyengelezya, Machi 2 mwaka huu saa 3.00 usiku karibu na nyumba ya marehemu.
Kwa mujibu wa Mwaruanda, uchunguzi wa awali umebainisha kuwa chanzo cha mauaji hayo ni mgogoro wa shamba la urithi, ambapo mtuhumiwa anadai marehemu na mama yao mzazi, waliuza shamba hilo kisha kugawana fedha peke yao bila ya kumshirikisha.
Akisimulia mkasa huo, Kamanda Mwaruanda amedai kuwa usiku huo wa tukio hilo, mtuhumiwa alijificha karibu na nyumba ya kaka yake huyo akiwa na shoka, akimsubiri arejee nyumbani kwake akitokea matembezini.
Inadaiwa Frank alimshtukiza kaka yake na kumkata kwa shoka kichawani hadi alipohakikisha kuwa amefariki ndipo akatoroka na kujificha kusikofahamika ambapo polisi wilayani Sumbawanga bado inamsaka.
Baadhi ya ndugu wa marehemu wakizungumza kwa nyakati tofauti na mwandishi, kwa masharti ya majina yao kutoaandikwa gazetini, wamethibitisha kuwa shamba hilo lililozua mgogoro kwa wanafamilia hao, liliachwa na baba mzazi wa vijana hao.
Pia wamethibitisha kuwa maziko ya ndugu yao yalifanyika kijijini hapo juzi saa 12.00 jioni.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, Jacob Mwaruanda, amethibitisha kutokea kwa mauaji hayo ya kikatili kijijini Fyengelezya, Machi 2 mwaka huu saa 3.00 usiku karibu na nyumba ya marehemu.
Kwa mujibu wa Mwaruanda, uchunguzi wa awali umebainisha kuwa chanzo cha mauaji hayo ni mgogoro wa shamba la urithi, ambapo mtuhumiwa anadai marehemu na mama yao mzazi, waliuza shamba hilo kisha kugawana fedha peke yao bila ya kumshirikisha.
Akisimulia mkasa huo, Kamanda Mwaruanda amedai kuwa usiku huo wa tukio hilo, mtuhumiwa alijificha karibu na nyumba ya kaka yake huyo akiwa na shoka, akimsubiri arejee nyumbani kwake akitokea matembezini.
Inadaiwa Frank alimshtukiza kaka yake na kumkata kwa shoka kichawani hadi alipohakikisha kuwa amefariki ndipo akatoroka na kujificha kusikofahamika ambapo polisi wilayani Sumbawanga bado inamsaka.
Baadhi ya ndugu wa marehemu wakizungumza kwa nyakati tofauti na mwandishi, kwa masharti ya majina yao kutoaandikwa gazetini, wamethibitisha kuwa shamba hilo lililozua mgogoro kwa wanafamilia hao, liliachwa na baba mzazi wa vijana hao.
Pia wamethibitisha kuwa maziko ya ndugu yao yalifanyika kijijini hapo juzi saa 12.00 jioni.