Majeruhi wa ajali ya basi la Morobest lililokuwa likitokea Mpwapwa kuelekea Dar es Salaam, wakiwa wamelazwa chini kusubiria huduma ya matibabu hospitalini. Watu 17 wamethibitishwa kufariki dunia mpaka sasa katika ajali hiyo ambayo basi hilo lenye namba za usajili T 258 AHV liligongana uso kwa uso na lori lenye namba T 820 CKU kwenye eneo la Pandambili, mkoani Dodoma mapema leo majira ya Saa 2 asubuhi.