Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Dodomainakusudia kuanzisha mfuko kutoa mafao maalumu kwa Watumishi wake baada ya kustaafu kazini.Katibu Mkuu wa Dayosisi ya Dodoma, Robert Mgaya alisema hayo jana wakati wa mahojiano na wanahabari juu ya kuanzishwa kwa mfuko huo.Alisema Halmashauri Kuu ya Dayosisi hiyo ilikaa Juni 12, mwaka huu chini ya Mwenyekiti wake Askofu wa KKKT Dayosisi ya Dodoma, Amon Kinyunyu na kukubaliana kupitisha mpango huo wa kuwasaidia watumishi hao baada ya kustaafu.Mgaya alisema sababu ya kuanzisha mfuko huo ni baada ya kuona watumishi wa kanisa hilo wanapostaafu maisha yao na familia zao kukosa mwelekeo na kuyumba kiasi cha kusikitisha.Alisema Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Dayosisi hiyo walitafakari kwa makini na kuona kuwa watumishi hao walilitumikia Kanisa kwa uaminifu, upendo na nguvu zao zote lakini mwisho wa siku hakuna anayewajali na kuishi maisha kama wakimbizi.Mgaya alisema Halmashauri Kuu ilikubaliana kuwepo na Jumapili moja kila mwezi kwa sharika zote na Mitaa ya Dayosisi hiyo kutoa sadaka maalumu kwa ajili ya mfuko huo kwa kiwango walichopangiwa.Aidha alisema katika kuhakikisha kuwa wamekusudia kuhusu kuanzisha mpango huo makanisa yote Julai 13, mwaka huu wataanza kufanya mchango maalumu kwa ajili ya kuzindua mfuko huo rasmi.Alisema Jumapili iliyopita wachungaji wote wa kanisa hilo walibadilishana vituo vyao vya kazi ili kuwahamasisha Wakristo wa makanisa yao juu ya kujiandaa kuanza kutoa michango ya kuanzisha mfuko huo.Mgaya alisema Kanisa lilikuwa likiwalipia watumishi wao katika mifuko ya kijamii lakini kutokana na mishahara yao kuwa midogo fedha hizo hazikidhi mahitaji yao baada ya kustaafu kutokana na kukabiliwa na majukumu ya kifamilia zao.
↧