Quantcast
Channel: ziro99blog
Viewing all articles
Browse latest Browse all 4529

BODABODA WATAKAOINGIA KATIKATI YA JIJI KUNYANG'ANYWA LESENI...

$
0
0
Waendesha bodaboda na 'bajaji'ambao watakiuka agizo la kutoingia katika Eneo la Katikati ya Jiji (CBD),  watanyang'anywa leseni zao za biashara, kwa kukiuka  sheria.

Hayo yameelezwa na Kamishna wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova wakati akizungumza na waandishi wa habari juu ya baadhi ya madereva wanaokiuka agizo hilo.
Alisema msako mkali wa kuwatafuta wanaokaidi agizo hilo unaendelea, hivyo kwa wanaokiuka hakuna atakayenusurika.
"Tunatoa onyo kali kwa watakaoendelea kukaidi agizo hili, kwani hatua kali zitachukuliwa ikiwa ni pamoja na kunyang'anywa au kufungiwa leseni ya kufanya biashara ya pikipiki na bajaji ndani na nje ya CBD," alisema Kova.
Alisema licha ya agizo hilo, operesheni iliyoanza Machi 10, mwaka huu mpaka sasa imeshakamata pikipiki na bajaji 1679, huku magari yakiwa ni 7958 na makosa yaliyokamatwa ni 9,937.
Alisema kutokana na operesheni hiyo wamefanikiwa kukusanya Sh milioni 298.11 ambazo zitapelekwa serikalini, aliongeza operesheni hiyo ni ya kudumu.
Aidha alisema katika msako wa kupambana na uhalifu, wamefanikiwa kukamata pikipiki 14 na bajaji moja ambazo ziliporwa na majambazi. Sambamba na watuhumiwa wanane wanaohusishwa na uhalifu huo.
Alitaja waliokamatwa ni Mafuru Joash (25), Salum Moes (22), Salum Ibrahim (20), Rashid Seif (30), Kasimu Ally (25), Hamza Juma (20), Mushi Kesi (34) na Abrahman Mussa (22) .
'Baada ya mahojiano watuhumiwa hawa walikiri kuhusika katika baadhi ya matukio ya ujambazi na kuonesha yadi ya magari iliyoko maeneo yua Mtoni Mashine ya Maji ambayo wanaitumia kuhifadhi pikipiki za wizi," alisema.
Mtuhumiwa Joash alikiri kuwa yeye ni mpokeaji mzoefu wa mali hizo za wizi na huwa anatafuta soko na kuziuza taratibu.

Viewing all articles
Browse latest Browse all 4529

Trending Articles