Quantcast
Channel: ziro99blog
Viewing all articles
Browse latest Browse all 4503

SHULE TATU ZA SEKONDARI ZAFUNGWA KWA UKOSEFU WA CHAKULA...

$
0
0
Wanafunzi wakijipatia chakula shuleni.
Shule  za  sekondari  tatu  za  bweni  mjini Sumbawanga zimelazimika kufungwa kutokana na  wanafunzi  kukosa chakula  baada  ya  wazabuni  kuzira  kuwasambazia  tangu  mapema  mwezi uliopita.

Hayo  yaliibuka  katika kikao cha Baraza la  Madiwani la Manispaa  ya Sumbawanga   mwishoni  mwa  wiki mjini hapa.
Shule zilizofungwa ni sekondari za Kantalamba, Sumbawanga na Kizwite, ambapo wazabuni  hao  wamesitisha  shughuli  zao  kushinikiza walipwe madeni yao ya tangu  Oktoba.
Wakichangia  kwenye  kikao  hicho  baadhi ya madiwani  walitaka  kujua lini  shule  hizo  zitafunguliwa  na  nini  hatima  ya  wazabuni  hao ambao  wamekuwa  wakisambaza  chakula  katika  shule  hizo.  
Uchunguzi uliofanywa na  mwandishi  wa  habari  hizi  umebaini  kuwa  wanafunzi  wa vidato  vya pili na nne walimudu kufanya mitihani  yao  ya kitaifa  hivyo waliokumbwa na  kadhia  hiyo  ni  wa vidato vingine.
Mkurugenzi wa Manispaa  hiyo, William Shimwela  alikiri wazabuni  hao kuacha kusambaza  vyakula  katika  shule  hizo  kwa  sababu  hawajalipwa   malipo yao  kutokana na kuchelewa  kufika  kwa  fedha.
"Naomba Baraza hili deni  la  wazabuni hawa  liletwe  kwenye  Kamati  ya Fedha  ili  kujadiliwa na kupatiwa  ufumbuzi," aliomba Shimwela.
Baadhi  ya  madiwani walionesha  masikitiko yao  kwa mji  wa Sumbawanga kupoteza umaridadi wa siku za nyuma kutokana na kukithiri kwa ujenzi holela unaofanywa na wakazi siku za karibuni.
Walieleza kuwa  dosari  hiyo  imesababishwa  na  Manispaa ya Sumbawanga kushindwa kugawa viwanja vipya vya ujenzi kwa muda mrefu kutokana na sababu mbalimbali.
Shimwela alisema tatizo la kutogawiwa kwa viwanja vipya linatokana na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Makazi kushindwa kupitisha ramani mpya za maeneo ambayo  yamekwishapimwa.
Alisema takribani miaka mitatu sasa wamekuwa wakipeleka ramani za maeneo ambayo yalishapimwa ili ziidhinishwe kabla ya wananchi kuanza kujenga, lakini hakuna kilichofanywa na Wizara husika.
"Hii inasikitisha kwani mji huu ulianza kujengwa kwa mpangilio mzuri lakini hivi sasa wananchi wanajenga nyumba ovyo na hii inatokana na kukata tamaa baada ya kusubiri kwa muda mrefu uamuzi wa Wizara husika kupitisha ramani za viwanja vya ujenzi", alisema Shimwela.

Viewing all articles
Browse latest Browse all 4503

Trending Articles