Mkazi wa kijiji cha Kisumba, Manispaa ya Sumbawanga, Halima Nambeya (18) ametupwa jela mwaka mmoja na Mahakama ya wilaya ya Sumbawanga baada ya kukiri kosa la kuiba mtoto mchanga wa kiume kwa lengo la kulinda ndoa yake ili asiachike kwa kukosa mtoto.
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, Frednand Rwegasira alisema mtuhumiwa huyo alimuiba mtoto huyo katika eneo la Jangwani mjini hapa na kumsafirisha hadi kijijini Kisumba nyumbani kwa babu yake.
“Halima alifikishwa mahakamani na kusomewa mashitaka ya wizi wa mtoto na alikiri kosa lake hilo na amehukumiwa kutumikia kifungo cha mwaka mmoja jela," alisema.
“Uchunguzi wa awali ulibainisha kuwa Halima awali alimdanganya mumewe alikuwa mjamzito hivyo anadaiwa kumuiba mtoto huyo mchanga ili amdanganye mumewe kuwa amejifungua kwa lengo la kulinda ndoa yake ili asiachike," alibainisha Kaimu Kamanda huyo.
Kwa mujibu wa Rwegarisa, Halima anadaiwa kutenda kosa hilo Juni 29 mwaka huu ambapo alikamatwa na Polisi siku nne baadaye akiwa nyumbani kwa babu yake kijijini Kisumba, Manispaa ya Sumbawanga.
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, Frednand Rwegasira alisema mtuhumiwa huyo alimuiba mtoto huyo katika eneo la Jangwani mjini hapa na kumsafirisha hadi kijijini Kisumba nyumbani kwa babu yake.
“Halima alifikishwa mahakamani na kusomewa mashitaka ya wizi wa mtoto na alikiri kosa lake hilo na amehukumiwa kutumikia kifungo cha mwaka mmoja jela," alisema.
“Uchunguzi wa awali ulibainisha kuwa Halima awali alimdanganya mumewe alikuwa mjamzito hivyo anadaiwa kumuiba mtoto huyo mchanga ili amdanganye mumewe kuwa amejifungua kwa lengo la kulinda ndoa yake ili asiachike," alibainisha Kaimu Kamanda huyo.
Kwa mujibu wa Rwegarisa, Halima anadaiwa kutenda kosa hilo Juni 29 mwaka huu ambapo alikamatwa na Polisi siku nne baadaye akiwa nyumbani kwa babu yake kijijini Kisumba, Manispaa ya Sumbawanga.