Quantcast
Channel: ziro99blog
Viewing all articles
Browse latest Browse all 4503

WAZINDUA KUMBUKUMBU YA MIAKA 20 YA MAUAJI YA KIMBARI...

$
0
0
Wapiganaji wa Intarahamwe.
Ubalozi wa Rwanda nchini umezindua kumbukumbu ya miaka 20 ya mauaji ya Kimbari na kuitambulisha kwa jina la Kinyarwanda kuwa ni Kwibuka20, ikiwa na maana ya kukumbuka.

Uzinduzi huo ulifanywa Dar es Salaam jana na Balozi wa Rwanda nchini, Ben Rugangazi  aliyeeleza kuwa uzinduzi huo ni sehemu ya maandalizi ya kumbukumbu rasmi ya mauaji hayo, itakayofanyika Aprili.
Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Balozi Rugangazi alisema kuwa wana Rwanda wamekuwa na umoja unaowafanya wawe kitu kimoja, hivyo kutofikiria kutengana tena kwa kuendeleza visasi.
Alisema, umoja huo umekuwa ukiendelea kuimarika kila siku, hivyo kuwafanya waliokuwa wakichochea mauaji na hata kuyawezesha kushindwa kupata nafasi ya kuurudia uchochezi wao.
Katika mauaji hayo ya mwaka 1994, kwa mujibu wa taarifa ya  Balozi Rugangazi aliyoitoa juzi, watu 10,000 walikuwa wakiuawa kila siku katika kipindi chote cha machafuko.

Viewing all articles
Browse latest Browse all 4503

Trending Articles